Chid Benz Kauza Mjengo Aliokuwa Anaishi na Kuhamia Kwa Mama Yake

Mwanamuziki wa Bongo fleva Chid Benz ameendelea kukaa kwenye headlines baada ya kupata skendo mpya ambapo inadaiwa kuwa ameuza nyumba yake na kuhamia kwa mama yake.

Kwa kipindi kirefu sasa Chid Benz amekuwa akiandamwa na skendo ya kutumia madawa ya kulevya ameshapelekwa Rehab lakini imeshindikana kuacha kutumia madawa.

download latest music    

East Africa Tv wanaripoti kuwa Chid Benz ameuza mjengo wa ghorofa aliokuwa anamiliki maeneo ya Ilala ambapo ndio ilikuwa makazi yake na hata ofisini kwake ambapo alikuwa na kundi lake la La familia.

Inadaiwa kuwa Chid ameuza mjengo huo na kufikia hatua ya kukosa makazi na hivyo kuamua kurudi kuishi nyumbani kwa mama yake.

Nimeuza nyumba yangu ya ghorofa na wala sio ya kwanza kuiuza, nimeuza nyumba nyingi na sasa ninaishi kwa mama yangu mzazi ambayo ni nyumba nimejenga mimi. Nimeuza ghorofa na nimeuza nyumba nyingi ambazo nilikuwa nazimilik na nitaendelea kuuza”.

Mapema mwaka huu jeshi la polisi mkoani Dodoma lilimshikilia msanii huyu baada ya kukamatwa na madawa ya kulevya aina ya heroin ambapo sio mara ya kwanza Chid kukamatwa na madawa ambayo ameshindwa kuyaacha.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.