Chid Benz Kufanya Ngoma na Jay -Z

Msanii mkonge wa miondoko ya hip-hop nchini, Chid Benz amefunguka na kusema kuwa mara nyingi amekuwa akisema vitu na watu wanashindwa kumuamini huku wengi wakisema kuwa anatumia madawa ya kulevya na ndio maana anakuwa anaongea vitu visivyokuwa na maana.

Akiongea na Clouds Tv, Chid Benz anasema kwa muda ule aliokuwa akiongea alikuwa hajalewa wala hajatumia kitu chochote ila anatoa taarifa kuwa anataka kuanza kufanya kazi na wasanii wakubwa wa nje kama Jay-z, Jada Pink, na hata 50 cent.

download latest music    

Mnaweza kusema eti  nimelewa pale niliposema kuwa nataka kufanya kazi na 2-pac, lakini ukweli ni kwamba hata ukiniangalia machoni ninaongea hapa waa sijalewa ila nina ngoma na jada pink,nina ngoma na 50 Cent, nimefanya ngoma na 2-Pac na nina ngoma na Jay Z pia.

Chid benz ambae bado masabiki wake wengi wamekuwa hawamwamini kutokana na ukweli kuwa wanahisi bado anatumia madawa amekuwa akitumia nguvu nyingi sana kuwa hakikishia kuwa hatumii madawa kwa sasa.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.