Christian Bella Awajia Juu Waliomposti Dimpoz Alipokuwa Mgonjwa Hoi Kitandani

Msanii maarufu wa muziki wa dansi nchini Christian Bella amewajia juu watu waliokuwa mstari wa mbele kumposti Ommy Dimpoz alipokuwa hoi kitandani lakini wakashindwa kumposti alipopona siku yake ya birthday.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Bella amesema alikuwepo wakati Dimpoz anaanza kuugua koo mpaka kufikia hatua ya kufanyiwa Upasuaji lakini amewalipua watu ambao walimposti Dimpoz wakati akiwa hoi kitandani na kumtakia apone haraka lakini alivyopona hawakufanya hivyo wala hawakuposti wimbo wake mpya aliouachia hivi karibuni.

download latest music    

Watu walikuwa na wasiwasi sana huenda chochote kikatokea kwa Dimpoz, walimposti sana wakimuombea apone, hadi wale ambao alikuwa haelewani nao walimposti. Baada ya hapo ikafika Birthday yake lakini hao watu hawakumposti, na hata juzi alivyotoa wimbo wake hawakumposti lakini angefariki wangemposti sana”

Ommy Dimpoz aliugua nusu ya kufa miezi Michache iliyopita mpaka kufikia hatua ya kupostiwa na kila Msanii akiwemo hasimu Wake namba moja Diamond Platnumz.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.