Christian Bella: Mimi na Alikiba ni Wahenga Ila Diamond ni Digitali

Msanii wa bongo fleva anayefanya mziki wa dansi nchini, Christian Bella amefunguka na kudai kuwa yeye na msanii mwenzake Alikiba ni wahenga lakini Diamond ni msanii wadigitali.

Hivi karibuni kwenye mahojiano na kituo cha televisheni cha East Africa Christian alidai kuwa yeye na Alikiba ni wasanii wazuri lakini hawawezi kupambanishwa katika kitengo kimoja kwani wanafanya mziki Mkubwa.

download latest music    

Christian Bella amepiga stori na Bongo 5 na amefunguka na  kuzungumzia ukongwe wake kwenye muziki bila kutetereka na kumsifia msanii mwenzake Alikiba na kudai kuwa Diamond  ni msanii wa digitali sio msanii wa zamani kama yeye na Alikiba.

Kwenye mahojiano hayo alifunguka yafuatayo:

Unajua wasanii kama Diamond, Belle 9 na wengineo walioingia kwenye gemu kuanzia mwaka 2010 ni wasanii wa digitali, lakini  mimi nampa sana saluti msanii mwenzangu Alikiba ambaye naweza sema ni mhenga kama mimi au msanii wa analogi mwenzangu maanaalianza kuhit kitambo sana yaani amevuka kutoka kwenye analogies mpaka sasa bado yupo anapambana na vijana wa kwenye digitali alafu mimi nakuja Tanzania  2005 namkuta Alikiba tayari ana-hit yaani supastaa ana ngoma nyingi zinapendwa kwaiyo ni artist mkongwe kwenye gemu kama mimi “.

Lakini Christian Bella amekiri kuwa Diamond ni moja kati ya wasanii waliokuza mziki wa bongo fleva tangu aingie kwenye gemu miaka ya 2010 kwani katika kipindi hicho mziki wa dansi ulikuwa umeitoa Bongo fleva kwenye ramani na hivyo Diamond aliurudisha mziki wa Bongo fleva kwenye chati na kuua mziki wa dansi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.