Christian Bella: Mimi ni Namba Moja Nisifananishwe na Alikiba

Mwanamuziki na mkali wa mziki wa dansi nchini, Christian Bella ameibuka na kudai kuwa yeye ni mwanamuziki namba moja na asifananishwe wala kupambanishwa na mkali mwenzie Ali Kiba.

Baada ya kipindi cha ‘cheche’ kuingia mtaani na kuhoji watu ili kuuliza watu nani mkali wa ‘vocal’ kati ya Ali Kiba na Christian Bella na majibu kurudi huku watu wengi wakimpigia kura Ali Kiba kuwa ni mkali kuliko Christian Bella na kuibuka mshindi kitendo ambacho Bella alionesha kutokuridhika na kusema Kiba ni mkubwa katika mziki wake wa Bongo fleva lakini na yeye mkubwa kwenye mziki wake wa dansi.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo cha televisheni cha East Africa, Christian Bella alifunguka haya kuhusiana na ushindindani huo dhidi ya Kiba.

Unajua huo ni mtazamo wa shabiki waliyemhoji huyo walimhoji anamkubali msanii wake kila msanii ana mashabiki wake na mimi najua watu mliowahoji wanaweza wakawa mashabiki wanaompenda Alikiba na mimi sijawahi kusema kuwa Alikiba sio msanii mzuri kwaiyo mtu akisema kuwa ni msanii mzuri siyo vibaya kwanza sijawahi kujali sijui umsifie mtu zaidi yangu eti nione vibaya?Noo ila kama mlipiga kura mkaona Kiba ni zaidi sio vibaya siwezi kukataa maoni ya wale ila ukweli wangu hata ukimhoji Kiba hawezi kusema kuwa ananishinda mimi hats siku moja never! Alafu Ali hawezi kunizidi mimi na mimi siwezi kumzidi yeye hata siku moja”.

Pia Bella amekiri kuwa ni vigumu kumshindanisha yeye na Alikiba kwa sababu wanafanya aina mbili za mziki zilizo tofauti kabisa na hivyo hawawezi kupambanishwa kwani Kiba anafanya Bongo fleva na yeye anafanya mziki wa Dansi na kila mmoja ni mkali katika kitengo chake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.