Chuchu Awatolea Povu Wanaomponda Kuwa na Ray Katika Mwezi Mtukufu

Muigizaji wa Bongo movie Chuchu Hansy amekuwa mbogo kwa watu wote wanaomsema yeye kuwa na ukaribu na mpenzi wake Ray Kigosi katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani ili hali yeye ni binti wa Kiislamu.

Chuchu na Ray wamekuwa Kwenye mahusiano ya kimapenzi kwa muda mrefu na wamejaliwa kupata mtoto mmoja lakini wawili hao hawajafunga ndoa ambapo ni kinyume maandiko ya dini ya kiislamu kukaa na mpenzi wako hasa kwa mwezi huu.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Global Publishers kwa njia ya simu akiwa nchini Afrika Kusini na mzazi mwenziye huyo kwa ajili ya kushuti filamu, alisema kuwa kuishi na mzazi mwenziye huyo kwa ajili ya kazi haoni kama ni dhambi lakini anashangaa watu wanavyotoa hukumu mitandaoni kwamba anakosea.

Mimi ninachojua wa kumhukumu mtu ni Mungu pekee kwa sababu yeye ndiyo anajua ukweli wote na anajua kila kitu cha binadamu na si mtu mwingine, najua nilivyo huku na Ray watu wanasema sana tu lakini sijali“.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.