Chuchu Hansy Afungukia Habari Za Mimba Yake Kuharibika

Msanii wa Bongo movie na mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Ray Vicent Kigosi, Chuchu Hansy amefunguka na kuongelea suala lake la mimba kuharibika.

Siku za hivi Karibuni Kumekuwa na tetesi kuwa Mrembo huyo Chuchu Hansy amekuwa katika kipindi kigumu mara baada ya mimba aliyokuwa amebeba kuchoropoka.

download latest music    

Chu­chu Hans ametoa povu baada ya kudaiwa kuwa alinasa ujauzito ukachoropoka akiwa nchi­ni Afrika Kusini alipokuwa na Ray kwa ajili ya matembezi ya kifamilia.

Kwenye mahojiano aliyofanya na gazeti la Ijumaa Wikienda, Chuchu alisema anawashangaa wa­naomfuatilia kila kukicha. Alisema ni ajabu kuona watu wanamfuatilia kama ana mimba au la.

Kila kukicha watu wanapenda ku­fuatilia mambo yangu na sijui ni kwa nini maana hata kama nikizaa watoto kumi na Ray, ni sawa kwa sababu ni mwanaume na ananipenda na kujali, kwa hiyo hata kama imetoka nitabeba tena hivi karibuni“.

Ray na Chuchu Hansy tayari wana mtoto mmoja wa kiume anayeitwa Jaden.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.