Chuchu Hansy Afungukia Tetesi Za Ray Kuwa Muathirika Wa Ukimwi

Muigizaji wa Bongo movie Chuchu Hansy amefunguka na kuongelea tetesi zilizowahi kukamata headlines kuwa Mzazi mwenzake na mpenzi wake Msanii Vicent Kigosi ‘Ray’ ni Muathirika wa Ukimwi.

Chuchu amefunguka na kudai kuwa alishawahi kukumbana na maneno mengi ya kejeli ikiwemo kusema kuwa amepewa ujauzito na mwanaume ambaye ni Muathirika wa Ukimwi.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Chuchu amefungukia tetesi hizo:

Nilishtushwa sana na maneno hayo ila unajua siku zote mwisho wa ubaya ni aibu kwa sababu toka waseme nina Ukimwi kupitia kwa Ray mpaka leo hii bado wananiona nadunda na wala sina hata dalili yoyote ya kuumwa”.

Chuchu aliongeza kuwa maneno hayo yaliwachukiza sana ndipo mzazi mwenziye (Ray) alipowaumbua kwa kuweka picha yake (Chuchu) mtandaoni akimnyonyesha mwanaye Jaden kuthibitisha kuwa, wote ni wazima na hapo ndipo wambeya likawashuka.

Kuna watu wengine mpaka sasa wanaona hata aibu kunitazama, wamesahau kuwa haifai kabisa kumnyooshea mwenzako kidole”.

Kwa miaka mingi kulikuwa na tetesi za Ray kuwa mgumba baada ya kutofanikiwa kupata mtoto lakini tetesi hizo zilikuja kuisha baada ya Chuchu kujifungua mtoto wao Jaden.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.