Chuchu Hansy Amedai Akiachana Na Ray Hataki Mwanaume Mwingine Tanzania

Muigizaji wa Bongo movie, Chuchu Hansy amefunguka na kudai kuwa endapo atakuja kuachana na mpenzi wake Ray Vincent Kigosi basi hataki mwanaume mwingine Tanzania.

Siku za hivi karibuni tetesi zimeenea kuwa Chuchu na Ray wameachana, wawili hao ambao miezi michache iliyopita walizaa mtoto wao wa kwanza wa kiume aitwae Jayden walisemekana kuwa kila mmoja kashika njia yake na kuenda kivyake taarifa zilizo thibitishwa na kutoonekana kwao pamoja wakipiga picha na kuweka kwenye mitandao ya kijamii kitu kilicho wafanya mashabiki zao waamini moja kwa moja kuwa wapendanao hawa wameachana.

download latest music    

Kwenye mahojiano waliofanyiwa na kituo cha televisheni cha East Africa kupitia kipindi cha Planet Bongo katika nyakati tofauti Chuchu na Ray wamekana tetesi hizo za wao kutengana. Huku Chuchu akisisitiza kuwa endapo ataachana na Ray hataki mwanaume mwingine Tanzania;

Kuachana kupo kwa sababu kila kitu Mwenyezi Mungu ndio anapanga, kwaiyo mimi siwezi kushindana na Mungu, basi kama ikitokea ndio itakuwa imefika mwisho wetu, Ila sidhani kama nitaweza kuwa na mwanaume mwingine hapa Tanzania, sidhani, yaani sidhani kama nitaingia kwenye mahusiano Tena, yaani nahisi nitakaa kwa muda mrefu sana bila mahusiano yoyote”.

Ray pia alikana tetesi hizo na kudai kuwa hana sababu yoyote ya kuachana na mpenzi wake Chuchu kwani ni mwanamke anayempenda sana.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.