Dadake Diamond – Queen Darleen akana kuwai kuwa mpenzi wa Ali Kiba

Kabla Diamond hajakua nyota Tanzania, Ali Kiba na Queen Darleen walikua marafiki wa dhati. Diamond aliponza kutawala kimuziki, Ali Kiba alianza uadui na yeye kisa kilichosababisha kusambaratika kwa uhusiano wake na Queen Darleen ambaye alisimama na kakake.

Ukaribu wa Queen Darleen na Ali Kiba ulichangia kuzuka uvumi kuwa wawili hao walikua wapenzi, madai ambayo dadake Diamond amepinga.

download latest music    
Queen Darleen na Diamond

“Sio kweli Alikiba hajawahi kuwa bwana wangu, Ali Kiba ni ndugu yangu na tuna heshimiana sana zaidi ya sana. Unajua mimi watu mpaka leo hawajua mwanamume wangu nani, kwa hiyo hata wewe naweza nikazunguka nawe wiki mbili halafu watasema ni wewe. Ali Kiba ni ndugu kabisa, ni mshikaji wangu na ndivyo ilivyokuwa tunazunguka naye sana. Ikumbuke kipindi kile nilikuwa nazunguna na Ali tayari nilikuwa mjamzito kwa hiyo kwa mantiki hiyo basi yule mtoto angekuwa wa Ali Kiba. Nimeambiwa watu wengi bwana angu hadi Dully Sykes wakati ni ndugu. Kipindi hata Nasibu (Diamond) anatoka tukawa tunazunguka naye kumsapoti, watu walisema tena ni bwanagu,” Queen Darleen aliambia EATV.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere