Daktari Aeleza Ugonjwa wa Ommy, Asema Uliwahi Kuwapata Watu Maarufu kama Maria Carey

Daktari wa maagonjwa ya koo, pua na masikio kutoka katika chuo kikuu cha muhimbili dokta godlove mfuko ameelezea matatizo yanayomkabili msanii wa muziki wa bongo fleva  ommy dimpoz kwa sasa na kusababisha afya yake kudhoofika sana.

Ommy dimpoz ambae mpaka sasa yupo nchini afrika ya kusini akiptaiwa matibabu ya ugonjwa wa koo ulisababisha kushindwa kumeza chakula na vimiminika hivyo kufanyiwa upasuaji inaripotiwa kuwa hali yake inadhidi kuimarika siku hadi siku.

download latest music    

Hata hivyo dakatari huyoa anaeleza kuwa ugonjwa huo umekuwa ukiwapata baadhi ya wasanii ikiwemo watu maarufi kama Marai Carey, Lauryn hills miaka ya hapo nyuma na kushindwa kuendelea na kazi zao za muziki kwa kipindi kirefu.

Daktari huyo anasema ugonjwa huo kitaalamu unaitwa dysphagia,  unaosababisha kupata maumivu sana kwenye koo wakati wa kula na kunywa  anasema ” matatizo yanayoweza kumpata mtu katika kushindwa kumeza chakula au vimiminika yapo mengi ikiwepo matatizo ya  kuziba kwa mfumo wa kupitisha chakula,uvimbe au saratani.”

“mwanzoni tunaangalia aina gani ya uvimbe kwa kipimo cha endoscopy lakini kama tutashindwa kuona vizuri basi tunapima kwa CT Scan , ambayo inaweza kutuonyesha vizuri uvimbe umeenda mpaka wapi.”

Kinyama kidogo utolewa katika koo na kupimwa kama ni saratani basi unatolewa kwa kufanyiwa upasuaji lakini kama ni uvimbe mdogo kweny umio tunaweza kukata  ili aendelee kumeza chakula vizuri.

Hata hivyo dakatai mfuko alipoulizwa kuhusu takwimu ya ugonjwa huo alisema kuwa tangu amekuwa mtaalamu wa magonjwa hayo hajawahi kupata mgonjwa mwenye tatizo hilo chini ya miaka 50, hivyo wengi wao sio watoto na vijana.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.