Darassa Ataja Sababu Iliyomfanya Akae Kimya

Msanii wa Bongo fleva aliyewahi kitikisa nchi na wimbo wake wa ‘Muziki’ Darassa CMG amefunguka na kuweka wazi sababu iliyompelekea kukaa kimya kwa muda wa mwaka mzima.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Kupitia mahojiano na  kipindi cha XXL cha Clouds Fmamefunguka kuhusu ishu ya ukimya wake wa mwaka mmoja ikiwemo tuhuma zilizokuwa zikiendelea mtaani juu yake baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu kwenye game ya Bongo Fleva.

download latest music    

Ni kweli nilikaa kimya sababu nilikuwa nimepata mtoto na muda wangu mwingi nilikuwa nautumia nikiwa nyumbani na hata hizo story ambazo zilikuwa zinaendelea juu yangu nilikuwa nazisikia nikiwa nyumbani kwangu huku nikiwa nimembeba mtoto wangu, Ilifika time watu walikuwa wanakuja kugonga nyumbani kwangu ili wanione je ni kweli yanayoendelea na ikawa inafika muda nafungua geti na nawauliza vipi mnaona nini”.     

Nimekaa ndani kwa mwaka mzima, Wasanii wengi wametoa ngoma zao na zimefanya vizuri, natumia fursa hii kumpongeza producer @abbah_process kwa kufanya ngoma nzuri ya Iokote, Watu wajue nimeanza kazi rasmi na ushindani utakuwa mkubwa”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.