Davina Akumbwa na Kashfa ya Utapeli

Staa wa bongo movie Halima Yahaya maarufu kama Davina amejikuta akiingia katika kashfa nzito ya kutapeli watu baada ya jina lake kutumiwa na watu wasiojulikana kutapeli watu katika mtandao wa facebook.

Davina ansema kuwa hakuna kitu kinamuumiza roho na kumsikitisha kama watu wanaotumia jina lake katika mitandao na kufanya utapeli kwa sababu mwisho wa siku sio kila mtu anaweza kuamini kuwa sio yeye anaefanya hivyo , ila kuna wanaojua kuwa yeye ndio tapeli.

download latest music    

kitendo cha huyo mtu kuwa anatumia jina langu kwa ajili ya kuomba ela kwa watu kimekuwa kikinisikitisha sana, na kimekuwa kikinitia doa sana kwa sababu mimi sijawahi kufanya kitu kama hicho hata mara moja.ninawaomba sana watu wae makini katika hilo kwa sababu huyo tapeli mkubwa anatumia vibaya majina ya mastaa.

Hii sio mara ya kwanza wasanii wamekuwa wakilalamika kuwa watu wengi sana kwa sasa wamekuwa wakitumia majina ya wasanii maaufu kufanya utapeli wa kuwaibia watu na mashabiki wamekuwa wakilalamikakwa sababu wanakuwa wanajua kuwa wanaofanya hivyo ni mastaa wenyewe. Katika swala hili hata Jackline Wolper pia alishawahi kuongelea na kusema kuwa jina lake limekuwa likitumia vibaya na hata namba zake za simu.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.