Davina Aweka Wazi Mipango Yake Ya Kuacha Kuigiza

Muigizaji mkongwe wa Bongo movie Halima Yahaya maarufu kwa Jina la usanii kama Davina amefunguka na kuweka wazi kuwa ana mpango wa kuacha kuigiza endapo atapata kazi ya kumuingizia.

Kwenye mahojiano aliyofanya na gazeti la Amani, Davina amesema kuwa sasa hivi ameanza biashara ya kuuza vitu mbalimbali vya urembo lakini yuko mbioni kuzindua na pafyumu yake.

download latest music    

Yaani biashara zangu zikikaa vizuri tu huwezi amini mambo ya kuigiza naweka kando  kabisa maana hakuna tunachopata kama sura tumeuza sana, kipindi hiki ni cha kutafuta pesa tu”.

Wasanii wengi wa Bongo movie wamekuwa wakilalamikia tasnia hiyo na kudai haina maslahi kwa wasanii wengi kuna ambao wamehamia Kwenye Bongo fleva na wengine kuacha kabisa kuigiza na kutafuta kazi za kawaida.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.