Daxo Chali Yuko Tayari Kufanya Kazi na Nini, ni Baada ya Kuachana na Nay

Mtayarshaji maarufu wa muziki nchini Daxo Chali amefunguka na kusema kuwa yeye hana kinyongo na kufanya kazi na mwanadada nini ambae hapo awali alikuwa akifanya nae kazi lakini alihama kwake na kwenda kufanya kazi na nay wa mitego.

Daxo Chali ambae ndie aliona vipaji vya Nini na Hytham mara ya kwanza na kuanza kufanya nao kazi lakini baadae walikuja kukorofishana sana baada ya Nini kujiingiza katika uhusiano wa kimapenzi na Nay wa mitego hivyo kutokuwa na nidhamu na kuwa akifanya yale anayojisikia hivyo kushindwana katika swala la kufanya kazi pamoja.

download latest music    

ata hivyo, baada ya muda Nini na Ney hivi karibuni walijitangaza kuwa wameacana huku sababu kubwa nini akisema kuwa wanawake wengi alionao nay wamemfanya aachane na Nay, Daxo Chali alipoulizwa kuhusu mahusinao hayo alijibu kuwa hajui swala la kuachana kwao kama ni kweli au kiki kwa sababu hata kipindi wapo katika mahusiano walikuwa wakikataa sana.

Daxo Chali aliulizwa kama angeweza kumpokea Nini tena kama atarudi kwake na yeye hakusita kusema kuwa kama nini atakuja kufanya kazi kwake atamokea kama wasanii wengine wanavyokuja na kulipa kiwango kinachotakiwa basi hana kinyongo cha kufanya nao kazi.

Daxo Chali anasema kuwa anafurahi kuwasaidia wasanii na kufikia muda wa kujitambua na kuamua kufanya kazi kama wao hivyo kwa Nini hakuwa na shida nae hata kidogo na ndio maana alimuacha aende.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.