Dayna Awalaani Wanaoenda Kudanga Nje ya Nchi

Mwanadada Mwanaisha Said maarufu kama Dayna amefunguka na kuwalaani wasanii wa kike ambao wamekuwa wakienda nje ya nchi tena hasa Marekani na kufanya kazi za kudanga na kuwafanya watu wa nchi hizo kuamini kuwa wasanii kutoka bongo wapo kwa ajili ya kufanya kazi hizo wanapoenda nje ya nchi.

Ilikiwisha wahi kuripotiwa kuwa wasanii wengi wa kike wamekuwa wakienda Marekani na kufanya biashara za ngono kitu ambacho kimekuwa kikiwaharibia soko wasanii wengine wanaokwenda kwa ajili ya kufanya kazi za musiki nchi humo.

download latest music    

Dayna amesema kuwa hata hivyo kwa muda mrefu amekuwa nchini Marekani kwa ajili ya kuangaika na kazi zake lakini itu cha kushabgaza ni kwamba kuna baadhi ya watu wamekuwa wakimjadili kuwa yupo huko kwa ajili ya biashara ya ngono kitu ambacho sio cha kweli hata kidogo.

Najua wapo wasanii wachache ambao wametuharibia kabisa  soko hasa tunapoenda nje ya nchi na hasa marekani,kuna nchini zingine watu wakituona wanaanza kutufikiria kuwa tumeenda kwa ajili ya kufanya biashara ya ngono wakati ilo sio kweli kwa mfano  kama mimi nilikuwa marekani kwa ajili ya kufatilia kazi zangu za muziki. Alifunguka Dayna.

Malalamiko ya Dayna yanaenda sambamba na tabia za wasichana wengi wa bongo hasa wasanii ambao wamekuwa natabia ya kwenda kudanga na kufanya biashra za ufuksa huku wakisambaza sifa mbaya kwa wasanii wengine kutoka Afrika.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.