Dayna Nyange Afunguka Kuhusu Kuumizwa na Mapenzi

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Dayna Nyange anayefanya vyema na wimbo wake wa ‘Salama’ amefunguka na kuzungumzia namna alivyotendwa na mwanaume ambaye alikuwa anatoka naye kimapenzi tukio lililomfanya aandike wimbo huo.

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Dayna amefunguka na kueleza wimbo wake mpya umetokana na mambo aliyoyapitia kwenye mahusiano yake ya mwisho ambayo aliishia kuumizwa vibaya mno na mwanaume aliyekuwa naye;

download latest music    

Mapenzi yanazingua sana ndio maana nasema ni bora mtu kuwa single kuliko kudate na kitunguu kila siku unalia, nilinusurika kuposti kitu tu juzi sema malaika wa kheri akaniambia sio wewe Dayna hebu acha nikaona haya mambo na maumivu bora nikayamalize studio.

Nikaenda tu studio nikatoa machungu yangu kwenye wimbo wangu unaoitwa ”Salama” lakini mimi ni binti ambaye nikIwa kwenye mahusiano nakuwa kwenye mahusiano ya muda mrefu sana kuanzia miaka mitano na kuendelea”.

Lakini pia Dayna amedai kwa sasa amegundua kwanini baadhi ya wasichana wanatoka kimapenzi na wanaume wazee kwani bora kuliko kuumiza kichwa na vijana ambao wanaishia kuumiza moyo wako.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.