Dayna Nyange Afunguka Kukoshwa na Rayvanny

Mwanamuziki wa kike wa Bongo fleva Dayna Nyange anayefanya vizuri na ngoma yake ya Salesale amefunguka na kusema amefurahishwa kwa kiasi kikubwa na msanii mwenzake wa Bongo fleva kutoka WCB Rayvanny.

Dayna amesema amekoshwa na msanii mwenzake Rayvanny hii ikiwa ni baada ya kumtaja katika nyimbo yake inayofanya vizuri ndani na nje ya Bongo ‘Makulusa’ ambao amemshirikisha msanii kutoka South Africa anayejulikana kama Dj Maphorisa.

download latest music    

Kwenye wimbo huo wa Makulusa kuna kipande ambacho Rayvanny amemtaja Dayna Nyange ambapo mashairi yake yanaimba hivii “Kipotabo kama Dayna, ana shepu ya birika she got ice cream China, hips from America My baby she is finna”.

Kipotabo Dayna Nyange

Kwenye mahojiano aliyofanya na Times Fm Kupitia kipindi cha The playlist, Dayna alidai labda pengine Rayvanny alimtaja kutokana na vitu anavyovifanya kuendana na ngoma hiyo.

Unajua Dayna amekuwa Kipotabo kwa muda mrefu hajawahi kuongezeka kwaiyo naamini Rayvanny akaona ngoja nimuweke Dayna kwa sababu huyu baadae hawezi kuja kunipa shida , na mimi kwa upande wangu nilifurahi sana japo kila nilikuwa nje ya nchi na sikutegemea kama alikuwa anaweza kufanya kitu kama hicho kwa sababu sikuwa na ukaribu naye kihivyo so I was happy”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.