Dayna nyange Aweka Wazi Tetesi za Kuwa Mjamzito na Baba Kijacho WakeN

Msanii wa kike  muziki wa bongo fleva Dayna Nyange amefunguka na kuwekawazi kwa tetesi zilizokuwa zikisambaa katika mitandoa ya kijamii kuhusu kuwa mjamzito.Dayna anasema kuwa kwa muda amekuwa akisikia kuwa watu wamekuwa wakisema kuwa yeye ni mjamzito lakini ukweli ni kwamba yeye sio mjamzito na wanaomzushia wanatakiwa wajue hilo.

Akiongea na mwandishi wa habari wa Clouds Tv, Tei .Dayna Nyange anasema kuwa siku ya Valentine alipost picha ikimuonyeshe kuwa anakitumbo kikubwa na kuwatakiwa watu Valentine njema lakini kitu cha ajabu ni kwamba baada ya post hiyo watu walianza kusambaza picha hiyo na kumtamkia kuwa yeye ni mjamzito.

download latest music    

Dayna anasema kuwa siku hiyo alikuwa tu ameshiba na kuamua kuweka picha hiyo katika mtandao lakini kitu cha ajabu anakuja kuona ilishasambaa na walishamtafuta hadi baba wa mtoto huyo wakati sio kweli.

kuna vitu sio lazima uweke wazi moja kwa moja,ikifika muda wa kujulikana basi itajulikana tu.mimi nilikuwa nimekula zangu maharage nimeshiba  nikapost lakini baada ya hapo watu wakaanza kusema kuwa  nina mimba na nini na nini.-Alifunguka Dayna.

Hata hivuo mwandishi alitaka kujua neno lake la mwisho kuhusu hali hiyo ambayo watu wamekuwa wakimtangazia katika  mitandao ya kijamii na Dayna Nyange kwa kigugumizi kizito alisikika akisema.

no comment kwakweli kuhusu hilo, siwezi kusema kama ipo au haipo.

Hata hivyo mwandishi aliamua kumuuliza kuhusu tetesi za kuwa mimba hiyo ya dayna ni ya producer kutoka nchi Kenya William Tuva,ambapo wiki iliyopita kupitia kipindi cha Shilawadu habari hzio ndipo zilipoanza kusambaa.

binafis sijui kwanini watu waliamua kumzushia tuvva,kwa sababu mimi sijawahi kuweka mahusiano yangu wazi, kwaio hata sijui kwanini.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.