Diamond Adaiwa Kufaidi Penzi La Mrembo Wa Kinyarwanda

Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz na CEO wa WCB ameingia Tena Kwenye skendo ya Kimapenzi na Mrembo kutoka Rwanda anayejulikana kama Shaddyboo.

Diamond ameshawahi kusemekana kuwa na mahusiano na Mrembo huyo siku za nyuma wakati bado Yupo na Baby mama wake Zari, ambapo ameonekana naye kila akienda nchini Rwanda kwa ajili ya shoo.

download latest music    

Tetesi za wawili hawa kuwa Kwenye Mahusiano zilianza mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya Shady Boo kuja Tanzania kwa ajili ya kuwa Host ya Jibebe Challenge ya Diamond Platnumz.

Shadyboo alichochea tetesi za kuwa kwenye mahusiano na Diamond baada ya kuposti video iliyomuonyesha akiwa hotelini ambako inasemekana ni chumba kimoja ambacho alionekana Diamond pia.

Lakini pia Shadyboo aliposti video Kwenye mtandao wa Instagram iliyomuonyesha akikata mauno balaa akicheza wimbo wa Jibebe wa Diamond.

Pamoja na tetesi kusambaa kuwa Diamond anafaidi Penzi la Mrembo huyo, hakuna aliyekiri wala kukataa taarifa hizo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.