Diamond Adaiwa Kumnyapia Nyapia Irene Uwoya

Staa wa muziki wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz amerudi tena kwenye headlines akihusishwa na mwanamke mwingine ambapo safari hii Malkia wa Bongo movie Irene Uwoya.

Siku ya jana Diamond aliwashangaza mashabiki zake baada ya kuposti picha ya Irene Uwoya katika ukurasa wake wa Instagram bila kuambatanisha na ujumbe wowote hali iliyopeleka mashabiki hao kukosa majibu.

download latest music    

Baadhi ya watu walimjia juu Diamond kwa kitendo kile na kudai anakuwa anakosea kwa sababu Irene ni mke wa mtu lakini pia anakuwa anamkosea heshima Dogo Janja ambaye ni msanii mwenzake lakini pia ni mume wa halali wa Uwoya.

Lakini pia kuna baadhi ya mashabiki walimvaa Uwoya kwa kitendo chake cha kulike picha ile ya Diamond kumaanisha kuwa anafurahia attention ile anayoipata kutoka kwa Diamond na hata kumwambia anamuonea mume wake Dogo Janja kwa sababu ni mdogo kwake.

Diamond tena alienda kulike na kukomenti makopa kopa kuonyesha amekubali tena picha nyingine iliyopostiwa na Uwoya. Kitendo hiki kimetafsiriwa tofauti tofauti na watu kwani wapo waliosema Diamond anafanya hivyo ili kupata kiki, ingawa hakuna aliyesema kitu chochote yote haya ni mawazo ya mashabiki.

Ikumbukwe siku za nyuma kuliwahi kusemekana kuwa Diamond ameshawahi kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na Uwoya.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.