Diamond Afunguka Kuhusu Skendo Zinazomkabili

Mwanamuziki Diamond Platnumz anayetamba na wimbo wake wa Halelujah amefunguka kuhusu skendo zinazomkabili mtandaoni. Mbali na wimbo wake kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio na televisheni Diamond amekuwa katika vichwa vya habari kwa ajili ya maisha yake binafsi.

Baada ya tetesi kuenea kuwa Diamond ameachana na Zari tangu juzi wasichana mbalimbali wamekuwa wakidhaniwa kutembea na Diamond.

download latest music    

Kwa kupitia ukurasa wake Instagram Diamond amefunguka kuhusiana na tuhuma hizo;

“Mara Diamond kamla huyu mara nasikia anatembea na yule, mara inasemekana juzi alikuwa na yule, yaani kila ukiamka limezuka jipya utadhani yangu ina sukari au nakojoa dhahabu… Hebu niacheni kidogo  Niko busy nahangaika kupeleka bongo fleva yetu duniani..Sijamkaza yoyote na wala sina mahusiano na yoyote anayetajwa na siku nikimaliza mahusiano na aliye South Africa na  nikawa na mwingine na ikafikia kuliweka wazi ntaliweka wazi mwenyewe….Maana hakuna kitakachonizuia….Ndo kwanza Nina miaka 28, sijaoa na hata nikioa naruhusiwa kuwa na wake wanne Period!”.

Baada ya kuweka maneno hayo katika ukurasa wake Zari Alimjia juu na kumuomba asimuingize katika mambo yao kwani hayupo nae tena.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.