Diamond Ahaidi Kutoa Misaada Kwa Kwa Watoto 300 man Wanawake 200 Tandale

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz amefunguka na kuweka wazi mipango yake ya kutoa msaada mkubwa Tandale kwa ajili ya kusheherekea Birthday yake.

Katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa, Diamond Platnumz ameahidi kulipia BIMA ya Afya kwa watoto 300, kutoa mitaji kwa akina mama 200, kutoa Boda boda 20 na kukarabati Shule zote za msingi zilizopo ndani ya Kata aliyozaliwa ya Tandale.

download latest music    

Diamond akiongea kwenye sherehe fupi iliyofanyika Live kupitia Wasafi TV, amesema kuwa siku ya Ijumaa Tarehe 5 Oktoba 2018 atatimiza ahadi hiyo ikiwa na pamoja kuchinja ng’ombe na kusherehekea na watu wake wa Tandale.

Jambo la kwanza kabisa ni kuzungumza na vijana wenzangu wa Tandale ili kuwapa maneno ya kuwatia moyo. Lakini pia nitatoa bima za afya kwa watoto wasiopingua 300 na pia nitatoa mitano kwa wanawake 200”.

Diamond ametangaza kusheherekea Birthday kwa muda wa wiki nzima.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.