Diamond Akiri Kumkubali Mrisho Mpoto Kwa Staili Yake Mpya

Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz amemvulia kofia  na kuonyesha kumkubali Msanii Mrisho Mpoto baada Ya staili yake aliyotumia kuimba wimbo alioshirikishwa na Harmonize unaoitwa Nimwage Radhi

Msanii Mrisho Mpoto ameshazoeleka kwa staili yake moja ya uimbaji aliyoitumia Kwenye nyimbo zake maarufu kama Mjomba, Zisonje na Njoo Uzichukue na nyinginezo.

download latest music    

Lakini Kwenye Wimbo Mpya alioshirikishwa na Harmonize ambao sasahivi unafanya vizuri sana Nimwage Radhi Mpoto amekuja kwa staili nyingine kabisa ya kuimba na kuwafurahisha watu wengi ikiwemo Diamond Platnumz.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Diamond ameshindwa kujizuia na kumwagia sifa Mrisho Mpoto ambapo ameandika:

Kwa kweli Mrisho Mpoto nilikuwa nakuwaza sana, Kwa ufanisi wa serikali hii, ungewezaje kutupa vile vibao vyako vya #MJOMBA #WAITE Na Kadharika…. ila nimeamini kweli Mungu kakutunuku Kipaji na Ubunifu wa Sanaa, Sikutegemea kama UtaniSurprise namna hii… #NimwageRadhi Kali sana?? ….Mdogo angu Mmakonde @harmonize_tz naona Mwaka Huu unahasira nao sana….Kama Naiona hiyo #WasafiFestival Huu Mwaka Sjui hata tuanzie Mkoa gani???,” aliandika Diamond Instagram“.

Wimbo huo umekuwa ukifanya vizuri na kushika chati katika vituo mbali mbali vya habari na hata kushika nafasi za juu katika mtandao wa Youtube.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.