Diamond Alitaka Kunioa Mke Wa Pili, Nilikuwa Tayari- Hamisa

Mwanamitindo na Msanii wa Bongo fleva Hamisa Mobetto amefunguka na kuweka wazi uhusiano wake na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Hamisa amekiri kuwa wakati anaanzisha Mahusiano na Diamond, tayari Diamond alikuwa Kwenye Mahusiano na Zari na walikuwa wamezaa watoto.

download latest music    

Kwenye Interview yake aliyofanya akiwa nchini Kenya, Mobetto amefunguka haya:

Wakati nakutana na Diamond nilijua kuna Zari na nilimuuliza, akasema mimi ni muislam na uwezo wa kuoa hata wanawake wawili,” alisema Mobetto. “Na mimi nipoo tayari hata kama ningekuwa nimeolewa halafu mume wangu anataka kuoa mke wa pili ningemruhusu“.

Hamisa alibeba mimba ya Diamond wakati akiwa Kwenye Mahusiano na Zari jambo lililoleta mtafaruku na kupelekea kuachana kwao mwishowe.

Baada ya Diamond kuachana na Zari alikuwa Kwenye Mahusiano na Mobetto Tena lakini Mahusiano hayo yaliingia doa kwani Hamisa ameishia Kwenye ugomvi mkubwa na Familia na Diamond na kuishia kuachana naye.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.