Diamond Aliweka Hadharani Penzi la Mavoko na Lulu Diva

Staa wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz ameliweka hadharani penzi la msanii wa Bongo fleva kutoka WCB Rich Mavoko na Lulu Diva.

Kwa muda mrefu kumekuwa na tetesi kuwa msanii wa muziki Lulu Diva na Rich Mavoko ni wapenzi ingawa wenyewe wamekataa mara kwa mara kuwa hawana uhusiano wowote.

download latest music    

Lakini Diamond ametoa siri hiyo ya muda mrefu na kulianika penzi hilo Hadharani baada ya kumposti Lulu kwenye ukurasa wake wa Instagram Ikiwa ilikuwa ni birthday ya Lulu  Diva.

Kwenye posti hiyo Diamond aliwataka Rich Mavoko na Lulu Diva waache kujificha na badala yake wakae na wazae mtoto wao:

Pamoja na wawili hao kukataa kuwa walikuwa hawana uhusiano wa kimapenzi lakini mara kwa mara picha zao zilisambaa mitandaoni zilizowaonyesha katika mapozi ya kimahaba.

Baada ya kupewa dongo hilo Lulu Diva alimjibu Diamond kuwa wanataka wajenge kwanza nyumba kabla ya kuanza kuzaa kuwa na familia.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.