Diamond Amewazuia Wasanii Wake Wa WCB Kutoa Albamu

Mkali wa Bongo fleva, Diamond Platnumz anayetamba na nyimbo yake ya ‘Halelujah’ ambaye pia ni miliki wa label ya Wasafi Classic Baby (WCB) amedaiwa kuwazuiwa wasanii wake kutoa Albamu.

Diamond ambaye yuko mbioni kuachia albamu yake ‘A boy from Tandale’ mda wowote kuanzia sasa amedaiwa kuwakataza wasanii wake kama Queen Darlene, Richi Mavoko, Rayvanny, Harmonize, Lava Lava kutoa albamu wenyewe na badala yake kutakiwa kumpisha Diamond atoe albamu ya kwake kwanza.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyoyafanya hivi karibuni  na kituo cha redio cha Magic Fm kwenye kipindi cha Daladala beats, Rich Mavoko amesema yeye pamoja na wasanii wengine ndani ya WCB walikuwa na mpango wa kutoa Albamu ila Diamond alipotoa taarifa kuwa ana mpango wa kutoa Albamu mwaka huu ilibidi wampishe.

Kusema ukweli mtu ambaye anatuchelewesha foleni yetu ni Chibu tu kwa sababu ni mtu wa kwanza kupata idea ya kuanza kuanza Albamu mwaka huu tulikuwa tunaliheshimu wazo lake sisi tukawa wa pili, kwa hiyo tangu zamani nilikuwa Nina wazo la kutoa kwa mwaka huu baadae tukakubaliana yeye aanze kutoa na mimi nifuate then wenzangu wote waje kutoa baadae kwa sababu watu tuna mingoma kibao ndani inasubiria foleni ya kutoka”.

Rich Mavoko amedai kuwa WCB wote walivutiwa na wazo la kutoa Albamu pale Diamond alipowaeelezea jinsi atakavyo kuja kuuza albamu hiyo ya ‘A boy from Tandale’.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.