Diamond Amfungukia Mazito Mama Yake Siku Yake Ya Kuzaliwa

Staa wa Muziki wa Bongo fleva Naseeb Abdul maarufu kama Diamond Platnumz amemfungukia maneno mazito Mama yake mzazi Bi. Sandra alipomtumia salamu za Kheri siku yake ya kuzaliwa.

Diamond aliandika ujumbe huo wa kum-wish mama yake siku ya kuzaliwa kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond amesema mama yake amepitia magumu mengi sana ikiwemo manyanyaso wakati akimlea hivyo hakuna mtu wa kumlinganisha na mama yake.

download latest music    

Nasikitikaga sana Wanapojaribu Kulinganisha Thamani yako kwangu na Mtu yoyote…Na kusahau kuwa pasipo wewe kunizaa na Kunilea kwa shida na tabu leo hii hakuna yoyote ambae angeniona wamaana….. Ikiwa wewe ndio Ulonifanya mie nikawa Duniani Basi you will always be My First priority then the rest will follow…Dharau na Manyanyaso Ulopitia kwenye kunilea Hakuna anayejua, Tabu na shida Ulizopitia kufanya hadi leo walau nionekane mtu mbele za watu.. eti mtu kirahisi tu anatokea na kukuringanisha na mtu… Mama MADALE is your House!!! na ikitokea kesho nimekufa pia NUSU ya Mali zangu zote ni zako”.

Diamond amekuwa muwazi juu ya mapenzi makubwa aliyonayo kwa mama yake, na Julai 7, 2018 Mama yake na Diamond Platnumz, Sandra anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.