Diamond Amtumia Salamu Mh.Naibu Waziri
Msanii wa muziki wa bongo fleva nchini diamond platinumz kufuatia kitendo cha Naibu Waziri kumfungia msanii mwenzake Roma kwa muda wa miezi sitabia kufanya kazi yoyote inayohusiana na muziki kwa kosa la kuimba wimbo ambao unasemekana kuwa na upotofu na hauna maadili katika jamii.
Huwezi kumfungia mtu kama roma kwa miezi sita,unajua kuwa anachangamoto gani?umeshawahi kutaka kuzitatua, unanifungia nyimbo nzangu umeshawahi kuchangia ni i katika muziki wangu , utamnunulia tiffah wewe pampers, simuogopi mtu hata kaka jela mimi nitaenda kwa ajili ya kuukomboa muziki .ntaitetea bongo fleva kwa sababu naijua kuliko anavyoijua yeye anaetufungia , sio unakuja unafungia bila hata kufanya research, anakuja na atatuacha sisi hapa.
Diamond ambae anaonekana kujiamini kuwa hata iweje lazima atasimama kwa ajili ya bongo fleva,pamoja na kwamba hata yeye ameathirika na kufungiwa lakini yeye anasema kuwa wala hajali kwa sababu hajapata taarifa rasmi juu ya kufungiwa kwa nyimbo zake zaidi ya kuziona habari katika mitandao ya kijamii.