Diamond Aomba Radhi Mashabiki Wake Kwa Kutokutokea Katika Shoo

Diamond Platinumz ,Akiwa kama Msanii mkubwa nchini  ameomba radhi mashabiki wake ambao walikuwa wamekaa wakimsubiri kwa hamu katika shoo iliyoandaliwa na Mh. Paul Makonda huku ikihusisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza kutoa vyuo vyote Dar Es Salaam , show hiyo ambayo ilikuwa ikifanywa na kushiriki kwa wasanii wengi wakubwa na wakongwe ilitegemewa kuwa Diamond atakuwa ni mmoja ya wasanii watao kwenda ku-perfom katika jukwaa hilo lakini haikuwezekana.

Siku iliyofuata Diamond Platinumz alitumia ukurasa wake wa instagram kuwaomba radhi mashabiki wake wote ambao hata yeye mwenyewe alitumia njia kubwa kuwahasisha waweze kutokea alafu yeye akashindwa kutokea.

download latest music    

Najua wengi mlikuwa ma shaulu ya kuona uwepo wangu   pale mlimani city jana.. ila amini kabisa kuwa hata mimi nilikuwa nina shauku zaidi ya ile ya kwenu, ya kuimba na kufurahi pamoja nanyi, na shauku iyo ilikuwa kubwa kuliko yenu na ndio maana nilitumia jitihada sana  kuwahamasisha ili muwepo kwa wingi katika tamasha hilo ili tufike kwa wingi pale , lakini kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wangu nilishindwa kufika pale,hivyo tusisononeke wala kuchukukia , naomba radhi  na kuwapa pole wale wote waliokwazika jana ,Inshallah Mwenyezi Mungu siku akiniandikia kuwa na nyie ntawaarifu-Alifunguka Diamond

Show iyo ilikwenda vizuri na kufana sana kutokana na uwepo wa wasanii wengi wakubwa na wakongwe akiwepo AY,Mwana FA, Fid Q, Lady jay dee, rich mavoko.Lakini katika tamasha hilo wasanii lady jay dee na mwana Fa walionekana kwa mara ya kwanza wakiwa wote jukwaani tangu walipokorofishana miaka mingi iliyopita na kupata mwaka huu.

Kushoto ni mwanadada Lady Jay Dee akiwa na Ay, kulia ni Mwana Fa na Lady Jay Dee katika show ya freshersparty

Ukumbi wa Mlimani City ulikuwa umefurika wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.