Diamond aonyesha jumba lake ambalo liko Nairobi

Diamond tayari anamiliki majumba ya kifahari jijini Dar es Salaam na Johannesburg, Afrika Kusini. Hit maker huyo pia ako na jumba lingine Nairobi.

Baba Tiffah ni miongoni mwa wasanii wenye utajiri mkubwa Afrika. Staa huyo wa Wasafi anapata mapato kutoka kwa muziki wake na biashara anazofanya.

download latest music    

Utajiri wa Diamond unadhihirika kwa majumba ya kifahari anayomiliki Tanzania na Afrika Kusini. Diamond alitumia bilioni kadha kununua jumba jijini Johannesburg.

Diamond akiwa kwa makao yake jijini Johannesburg, Afrika Kusini

Diamond amesisimua watu kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuonekana akionyesha jumba lake jijini Nairobi, Kenya kwenye video.

“My apartment in Nairobi, call me Mr. Naseeb when am on these type of mission, not Diamond,” Baba Tiffah aliandika kwa video yake.

Tazama video hio hapo chini:

https://www.youtube.com/watch?v=kwqyKzPZAVk

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere