Diamond Ataja Siku Wasafi Fm Itaanza Kurusha Matangazo Yake

Staa wa muziki wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz amefunguka na kutaja tarehe ambayo Wasafi Fm, itaanza kurusha matangazo yake rasmi.

Mwaka jana mwishoni Diamond Platnumz ambaye sio msanii tu bali Mfanyabiashara pia alitangaza kuwa anaingia Kwenye ulimwengu wa Media kwa kufungua radio station na television station ambazo ni Wasafi Tv na Radio.

download latest music    

Diamond Platnumz amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu ni lini kituo chake cha radio cha Wasafi FM kitaanza kurusha matangazo kama ilivyo kwa kituo chake cha Runinga cha Wasafi TV.

Kwenye mahojiano yake na kituo cha radio cha Mayotte la 1ère cha kisiwani Mayotte ambapo yupo anafanya shoo Diamond alifunguka:

Nimefungua Tv inaitwa Wasafi TV na inafanya vizuri sana na tupo katika mikakati ya kuhakikisha inapatikana bara zima la Afrika na ulimwenguni kote. Lakini pia mwezi wa kwanza au mwishoni mwa mwaka huu tunafungua pia Wasafi FM itakuwa hewani”.

Wasafi Tv imekuwa hewani kwa kama Miezi miwili hivi na tayari imepata mafanikio makubwa sana ingawa haijaanza hata kurusha vipindi Rasmi na hata matangazo ya wadhamini lakini kwa maangalizo ya awali inaonekana Wasafi Tv inapita katika njia sahihi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.