Diamond Atangaza Kuja na Reality Show Ya Maisha Ya WCB

Staa wa Muziki wa Bongo fleva na CEO wa label ya WCB m, Diamond Platnumz amethibitisha ujio wa reality show kitakachoonyesha maisha halisi ya Label yake ya WCB.

Diamond ametumia ukurasa wake wa Instagram kutoa habari hiyo njema kwenda kwa mashabiki zake.

download latest music    

Kipindi hiko ambacho kitaonyesha maisha halisi ya kundi Zima la WCB kinatarajiwa kurushwa Wasafi Tv hapo siku za mbeleni.

Diamond alitoa taarifa hiyo alipokuwa njiani kuelekea nchini Uingereza ambapo anaenda kupiga shoo yake ya ‘A boy From Tandale’ ambapo aliandika:

Moja ya kitu ambacho nakisubiri kwa hamu ni ndani ya Wasafi Tv ni reality show ya WCB Wasafi…..wacha wamalize kutest signal zao wamwage maji tuoge kama kambale…. Na mnatujuaga siye hatujui kuficha yote mtayaona”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.