Diamond Atapata Tabu Sana :- Baba Diamond
Baada ya siku kadhaa kupita baada ya Diamond kuweka picha ya baba yake na mama yake pamoja na yeye bado akiwa mdogo lakini bado baba huyo anasema kuwa Diamond anayafanya hayo anayoyafanya kwa sababu yeye yuko hai.
Diamond ambae inaonekana kuwa anamchukia baba yake na baba yake anakiri kulijua hilo , amasema kuwa anajua kabisa kuwa Diamond anamchukia lakini anajua kuwa siku akifa ndio atajua umuhimu wake na kwamba itampa tabu sana atakapo kufa yeye
Niliiona hiyo picha na niliiona ni vizuri na nilijisikia faraja pia,haina tatioz lolote lakini mimi ninajua kabisa kuwa diamond ananichukia lakini hata iweje mimi ni baba yake, na ananichukia kwa sasa lakini ipo siku nikifa atapata tabu sana.
Baba diamond anasema kuwa pamoja na kwamba yeye ni baba ya Diamond lakini hajawahi kusaidiwa kama anavyostahili kama mzazi.