Diamond Atinga BASATA Kwa Ajili Ya Kesi Ya Mavoko

Staa wa Muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz na Mkurugenzi wa kampuni ya Wasafi amefika katika ofisi za Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa ajili ya madai ya aliyekuwa msanii wake Rich Mavoko.

Rich Mavoko alimburuza Diamond na Label nzima ya WCB mbele ya BASATA kwa madai ya mkataba wa kinyonyaji waliompa wakati amesainiwa chini ya Label ya WCB.

download latest music    

Diamond aliongozana na Mameneja wake wawili, Hamis Taletale ‘Babu Tale’ na Sallam Sharraf katika ofisi hizo mapema leo ili kuitikia wito.

Kwenye mahojiano na Global Publishers mmoja wa meneja wa Diamond, Sallam, amesema waliitwa na Basata na sasa wapo katika mazungumzo ya kutatua jambo hilo na kufikia mwafaka.

Sallam amesema ni vyema watu wakasubiria yatakayoamuliwa huko, ambapo wanaamini Basata itauambia umma nini kilichoafikiwa badala ya wao  kuwa wasemaji.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.