Diamond Atokwa na Povu Zito Baada ya Tetesi za Kurudiana na Wema Kutapakaa

Mwanamuziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz amewatolea povu zito watu wote ambao wamemtemea cheche siku ya jana baada ya tetesi za yeye kurudiana na Wema Sepetu kutapakaa kwenye mitandao ya kijamii.

Diamond alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Wema miaka minne iliyopita lakini baada ya kuachana urafiki uliisha na waligeuka maadui wakubwa sana kwa kipindi kirefu lakini baadae wawili hao walisema wamemaliza tofauti zao na wamekuwa marafiki.

download latest music    

Siku ya jana mitandao ya kijamii yote ilitawaliwa na skendo za Diamond na Wema ambapo picha na video zilizosambaa mtandaoni ziliwaonyesha wawili hao wakiwa wamekumbatiana na kupapasana na hata kuna muda Wema alitaka kumpiga busu Diamond.

Baada ya kuongelewa sana na watu kumponda Diamom kwa kuanzisha ukaribu ule na Wema wakati anajua wazi kuwa ana familia yake anayoiumiza hasa mpenzi wake Zari.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Diamond aliwatolea povu Kali wote waliomtolea cheche baada ya habari za yeye na Wema kutapakaa:

Wengi hupenda kuona watu wakiwa kwenye vita au uhasama usio na kichwa wala mguu eti utamsikia mtu anasema “Dogo mimi shabiki yako Mkubwa na ninaukubali sana ila kitendo cha kumualika Wema ‘umeniuzi’ kwa iyo wewe unataka mimi niendelee kuwa na vita na Wema ili iweje? Yaani nikiwa na vita na Wema wewe unafaidika nini? ama itasaidia vipi kwenye sanaa yetu? Huwezi kuwa shabiki yangu alafu unafurahia mimi kuwa na vita na mtu tena vita ambayo imeshaisha…Nina familia yangu naipenda naiheshimu…ila hiyo sio sababu ya kuwa na vita na watu na huu mfano mwingine unafuata…shukrani sana madam kwa kuja usiku wa Jana”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.