Diamond Kutumia Zaidi Ya Milioni 465 Kwa Ajili Ya Misaada Tandale

Siku ya Ijumaa staa wa Bongo fleva Abdul Naseeb maarufu kam Diamond Platnumz anatarajia kutoa missada kwa Wakazi wa Tandale siku ya Kesho.

Katika kusheherekea siku yake ya kuzaliwa Diamond ametangaza kuwa ana mpango wa kutoa msaada mkubwa kwa Wakazi wa  ukifikia jumla ya shilingi 465.

download latest music    

Muimbaji huyo amedai atatoa bima za afya kwa kaya 250, ambapo kila kaya ni tsh milioni 1501200 kwa bima ya NHIF. Kwa maaana hiyo kwa kaya 250 atatumia zaidi tsh milioni 375.

Pia atatoa mitaji ya biashara kwa akina mama ambapo inakaridiwa atatumia zaidi ya tsh milioni 20 kwa akina mama 100. Alisema atagawa tsh laki moja mpaka laki mbili kwa akina mama wa Tandale.

Amesema atatoa pikipiki 20 kwaajili ya vijana ili wajikwamue kiuchumi ambapo inakadiriwa atatumia zaidi ya tsh milioni 50.

Diamond amesema atakarabati shule za Tandale pamoja na kuweka matanki ya maji ambapo ninakadiriwa atatumia zaidi ya tsh milioni 50.Kwa maana hiyo huwenda muimbaji huyo akatumia zaidi ya tsh milioni 465 kwaajili ya kutekeleza ahadi zake hizo.

Diamond amefunguka kuwa ni muhimu kwake kwenda kutoa msaada Tandale kwani ndipo alipotokea katika maisha ya ukata.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.