Diamond- Mtoto Wa Hamisa ni Mtoto Wangu Kama Walivyo Watoto Wa Zari

Staa wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz amemwaga povu zito kwa mashabiki waliokuwa wanamnanga mtoto mmoja ale aliyezaa na Hamisa wakidai sio mtoto wake.

Siku ya jana Diamond aliachia trailer mpya ya shoo yake ya ‘The real Life of Wasafi’ itakayoonyesha maisha halisi ya familia ya Diamond itakayorushwa Kwenye Wasafi Tv.

download latest music    

Kwenye trailer hiyo kuna kipande kinachomuonyesha Diamond akiwataka anazungumzia watoto wake lakini watoto wanaoonekana ni wawili tu ambao amezaa na Zari huku mtoto wake aliyezaa na Hamisa hakuonekana.

Kuona hivyo mashabiki wa Zari wakaanza kumnanga mtoto wa Hamisa kuwa sio mtoto wa Diamond ndio maaan hajaonekana kwenye trailer ya shoo ile na hapendwi kama watoto wa Zari wanavyopendwa.

Baada ya maneno mengi sana Diamond alishindwa kujizuia na kuandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kuwa Dylan ni mtoto wake kama walivyo watoto aliozaa na Zari walionekana kwenye trailer ile sababu pekee ambayo ilisababisha mpaka Dyalan hakuonekana ni kwa sababu hakuwa na clip yake:

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.