Diamond- Mwanamke Mvuto wa Sura Kwanza Tabia Baadae

Staa wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz amefunguka na kudai kuwa akiwa anatafuta mwanamke anaangali sura kwanza mambo ya Tabia yanafuata baadae.

Diamond ameweka wazi kuwa kigezo chake kikubwa anachotumia katika kusaka mwanamke wa kuoa kwanza ni sura na sio Tabia kama wengi wanavyodai.

download latest music    

Kwenye mahojiano yake na kipindi cha Kaa Hapa cha TBC 1, Diamond ameweka wazi kuwa yeye anaangalia sura zaidi kwa sababu sura huwezi kuibadilisha lakini tabia unaweza ukmbadilisha mwanamke.

Kiukweli tabia tunapenda lakini wakati mwingine sura nazo zina uzito wake, Kiukweli tabia mnaweza kuelekezana ila sura kuelekezwa mtaelekezana vipi?. Tabia tunajifunza kama alijifunza kuchukia atajifunza kupenda, sura atajifunza vipi?, Kwa mwanamke mimi naangalia sura kwanza , tabia tutaelekezana”.

Lakini pia Diamond amesema kuwa kama angetoa asilimia kwa vigezo vya sura na tabia basi asilimia 70 angetoa kwa upande wa sura na asilimia 30 zilizobaki ndio angeangalia tabia.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.