Diamond na Bob Junior Watangaza Kuja Na Kazi Mpya

Staa wa muziki wa Bongo fleva na CEO wa WCB, Diamond Platnumz na msanii mwenzake na producer kutoka Sharobaro Records Bob Junior wametangaza kuja na project mpya.

Diamond na Bob Junior ambao kwa muda mrefu wamekuwa na tofauti wameonekana kuzimaliza tofauti hizo na kuamua kufanya kazi pamoja kama zamani.

download latest music    

Siku ya jana kuna kuna video clip ilisambaa Kwenye mitandao ya kijamii iliyomuonyesha Diamond na Bob Junior wakiwa pamoja na kuwataka mashabiki kukaa mkao wa Kula kwani kuna kazi wanafanya pamoja

Wasanii hao wawili walikuwa na tofauti kipindi cha katikati kwani maelewano yao hayakuwa mazuri kutokana na kutofautiana kikazi, lakini hivi sasa wasanii hao wanaonekana kuwa katika nafasi nzuri.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.