Diamond na Hamisa Warudi Mahakamani Tena Leo

                                         

                               Diamond akiwa anaingia mahakamani mapema leo.

download latest music    

Msanii wa muziki wa bongo fleva nchini na boss wa kundi la WCB, Diamond Platinumz ameonekana leo tena mahakamni na mzazi mwenzie Hamisa Mobeto. Ambapo wiki iliyopita walikuwa  mahakamni hapo kwa ajili ya usuhuishi wa kesi yao ya matunzo ya mtoto wao.

Hata hivyo wiki iliyopita wawili hao baada ya kutoka mahakamani walikiri na kusema kuwa kesi hiyo imeenda poa na walishakubaliana kumlea mtoto huyo kwa pamoja na kwa kushirikiana hivyo hakuna tena malumbano ya malezi kati yao kuhusu  mtoto wao.

Diamond na Hamisa waliponekana leo mahakamani , taarifa zinasema kuwa waliamua kuja mahakamni hapo kwa ajili ya kuweka kumbukumbu ya makubaliano na usuluhishi wao ili baadae isije kusumbua au kuonekana kuwa ni waongo.

Diamond alisema kuwa  mara ya mwisho kukutana haikuwa kesi bali ilikuwa ni kufanya usuluhishi ambapo leo tumekuja kuweka rekodi ya makubaliano hayo ili yasije yakazushwa mengine ya uongo na kweli.

Wawili hao walifikia hatua ya kupelekana mahakamani baada ya msanii huyo kutokuwa na maelewana na hamisa ambae ameweza kupata nae mtoto mmoja wa kiume  na kushindwa kuwa anatoa ela ya matumizi kwa ajili ya mtoto wake.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.