Diamond na Harmonize Wapania Kuondoa Muziki Wa Nigeria Bongo

Staa wa muziki wa Bongo fleva kutoka label ya WCB Diamond Platnumz na Harmonize wamekuja na mkakati wa kuua kabisa muziki wa Nigeria ambao umeshika sana kasi nchini Tanzania.

Harmonize amefunguka na kudai wimbo wake mpya wa Kwa ngwaru ni mwanzo mzuri wa kurudisha muziki wa kuchezeka Tanzania ambao kwa kipindi kirefu ulishikiliwa na muziki wa Bongo fleva.

download latest music    

Harmonize amefunguka Kwenye Interview aliyofanya na Radio Five na kudai kuwa nyimbo za kuchezeka Bongo zimepungua kwani ambazo zinazotoka sasa hivi zimepoa kitu ambacho kinafanya nyimbo za wasanii wa Nigeria kupewa nafasi hasa club.

Inafikia wakati tunaona ni lazima tucheze, so tukaona this time around tukija na Kwa Ngwaru kama ngoma nyingi zilitoka kama zimelala ndio maana ukienda club unasikia Wanigeria wakati sisi tunaweza tukafanya muziki mzuri watu wakapenda na wakacheza.

Mwisho wa siku tunapenda tu ngoma zao kwa sababu ya beat lakini lugha hatuijui”.

Harmonize alitoa wimbo huo wa Kwa ngwaru wiki iliyopita na ulitrend kwa wiki nzima Youtube, huu ni wimbo wa pili kwa Harmonize kumshirikisha Diamond ambapo wimbo wa kwanza ilikuwa ni Bado ambao ulifanya vizuri sana.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.