Diamond na Rayvanny Waomba Msamaha BASATA na Serikali Baada Ya Kufungiwa

Wasanii wa muziki wa Bongo fleva kutoka Katika Label ya WCB Diamond Platnumz na Rayvanny ameibuka na kuomba Radhi kwa serikali na BASATA siku chache Baada ya kufungiwa.

Wiki iliyopita Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) walitangaza kuwafungia wasanii Diamond Platnumz na Rayvanny Baada ya kukaidi amri yao na Kuperfom wimbo wa Mwanza uliofungiwa kwenye tamasha lao la Wasafi Festival.

download latest music    

BASATA Walitangaza kulifungia tamasha la Wasafi Festival na pia kuwataka wasanii hao kutoperfom katika nchi nyingine yoyote pamoja na kwamba walishapanga kwenda Kuperfom Nchini Kenya.

Lakini Wasanii hao wameomba msamaha Kwa BASATA na Serikali kwa ujumla na kuomba wasemehewe adhabu yao waliyopewa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Rayvanny ameposti kipande hiki cha video kinachoonyesha wasanii Hawa wakiomba radhi:

https://www.instagram.com/p/BroqbY3j9YE/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=1uqh6m3umbdj1

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.