Diamond na Vannesa Kuwania Tuzo Uingereza Tena
Wasanii wanaofanya vizuri sana tanzania katika kutangaza muzikiwa bongo ndani na nje ya nchi mabo kwa sasa wamekuwa kama kaka na dada wa bongo fleva Vannesa Mdee na Diamond Platinumz wameingia katika headlines tena baada ya kuwekwa tena katika tuzo za huko uingereza wakiwa na wasanii wengi wakubwa.
Tuzo hizo za African Pride 2018 zitakazo fanyika June 3 mwaka huu kutakuwa na wasanii wengine wangi kutoka afrika ambao watachuana vikali na wasanii wetu kutoka Tanzania.
Wasanii kama Tiwa Sawage, Yamei Alade, Kiss Daniel , Patoranking, Davido, Wizkid na wengine wengiwatakuwepo kutafuta msanii vora wa muziki afrika kwa upande wa kike na upande wa kiume.
Vannesa na Diamond sio mara yao ya kwanza kuwania tuzo mbalimbali za nje ya nchi na kutoka na ushindi wa kuwapa tanzania hshima juu ya muziki, hivyo kila la kheri kwa wasanii hawa lakini pia pale wanapohitaji sapoti mashabiki wawe mstari wa mbele kufanya hivyo.