Diamond na Wema Wabambwa Ndani ya Mahaba Mazito hadharani (picha na video)

Msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz amezua gumzo siku ya Jana baada ya kuonekana hadharani na aliyekuwa mpenzi wake muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu huku wakionekana wakiwa wanashikana shikana .

Diamond na Wema waliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi miaka kadhaa iliyopita lakini waliachana mwaka 2014 ambapo Diamond aliendelea na kuanzisha mahusiano na mzazi mwenzake Zari na Wema aliendelea na wanaume wengine.

download latest music    

Siku ya Jana label ya Diamond WCB iliandaa hafla kwa ajili ya kumtambulisha msanii wao mpya Marombosso au maarufu kama Mbosso aliyekuwa kwenye kundi la Yamoto Band.

Tafrija hiyo ilifanyika katika hoteli ya Hyatt Regency Hotel ambayo ilihudhuriwa na mastaa kibao akiwemo Wema Sepetu, ambaye alionekana akiwa beneti na rafiki yake Aunty Ezekiel.

Lakini baada ya muda macho yote yalikuwa kwa Wema na Diamond kwani katika hali iliyowashangaza wengi ukumbini hapo Diamond alianza kukumbatiana na Wema na kushikana shikana nywele na kupapasana migongo.

Baada ya picha hizo na video kusambaa na kila mmoja kuongea lake Mange Kimambi alifunguka na kusema kuwa Wema na Diamond wamerudiana na inavyosemekana hivi sasa ni kuwa Wema ana ujauzito wa Diamond na ndio maana Wema anamchukia sana Hamisa hiyo yote ni kwa sababu ya kuzaa na Diamond.

Mpaka sasa haijajulikana Zari na Diamond wanasimama wapi kama Wema na Diamond wamerudiana kati ingawa hakuna aliyethibitisha taarifa hizo mpaka hivi sasa ingawa Zari aliposti video akiwa kanisani siku ya jana.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.