Diamond Ndio Msanii Mwenye Mafanikio Yanayoonekana- Baraka The Prince

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vyema kabisa na ngoma yake ya ‘Sina’ Barakah The Prince amefunguka na kumtaja Diamod kama Msanii Mwenye mafanikio ambaye yanaonekana.

Barakah amemtaja Diamond baada ya kuulizwa kuhusu wasanii mwenye mafanikio ambapo amekiri kuwa wasanii kadhaa wenye mafanikio sana lakini Diamond ndiye anayeonekana kufanikiwa zaidi.

download latest music    

Kwenye mahojiano na kipindi cha The Playlist cha Times Fm, Barakah amesema wasanii wenye mafanikio wapo wengi lakini hajui mkwanja wao benki au hawajionyeshi sana lakini Diamond anaonekana wazi kabisa:

Wasanii wengi wana mafanikio wakina Ali Kiba, AY, Joti, Masanja, sitaki kujudge kama Diamond ndio Msanii wa kwanza kwa sababu sijui akaunti yake lakini kwa nje kila mtu anaweza kuwa na mtazamo huo kwa sababu anafanya vitu vinavyoonekana katika jamii”.

Barakah aliendelea kufunguka kuwa:

Lakini hatuwezi kusema nani namba moja kwa sababu hatujui akaunti ya Sugu ipoje? Ommy Dimpoz, Profesa Jay, Juma Nature na wasanii wengineo”.

Msanii Chemical amewahi kumtaja Diamond kama Msanii Mwenye mafanikio na pesa zaidi Kwenye muziki wa Bongo fleva.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.