Diamond Platnumz adaiwa kodi ya zaidi ya Sh. milioni 400

Hitmaker wa Nasema Nawe Diamond Platnumz amejipata kwenye matata baadaya mbunge wa Kinondoni, Maulid Mtulia kudai kuwa msanii huyo anadeni la Sh. milioni 400 analodaiwa na Mamlaka ya Mapato (TRA).

Akizungumza bungeni Maulid Mtulia aliweka wazi kuwa msanii huyu amekuwa akikwepa kulipa TRA kitu ambacho wasanii wakubwa kama yeye hufanya. Mazungumzo haya yalifanyika bungeni wakati wa mjadala wa bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

download latest music    

Diamond Platnumz anadaiwa pesa hizi kwani yeye ni mmoja wa wasanii ambao wanaoingiza pesa nyingi kupitia nyimbo zake lakini inaonekana muimbaji huyo amekuwa akikwepa kupeana pesa hizi kama inavyohitajika kila mwezi.

Hata hivyo Diamond Platnumz hajazungumzia swala hili ambalo limewaacha Watanzania kama wameshangaa.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua