Diamond, Rayvanny na Mbosso Wapata Ajali Stejini Sumbawanga (+Video)

Msanii wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB Diamond Platnumz na wasanii wenzake Rayvanny na Harmonize walipata ajali katika Steji ya Wasafi Festival iliyokuwa inafanyika mkoani Sumbawanga.

Shoo hiyo ilifanyika siku ya jana 9 Desemba katika uwanja wa Nelson Mandela ambapo wasanii hao walikuwa wanaperfom wimbo wao pendwa kabisa wa ‘Zilipendwa’ lakini ndipo balaa lilipotokea Baada ya wasanii hao kula mieleka.

download latest music    

Lakini baada ya kudondoka kwa Diamond akifuatiwa na Mbosso wasanii hao waliinuka na kuendelea na shoo na iliripotiwa kuwa hakuna Msanii aliyepata majeraha makubwa zaidi ya michubuko ya hapa na pale.

Meneja wa Diamond Platnumz, Babu Tale alitoa taarifa kuwa wasanii hao wanaendelea vizuri na hakuna aliyeumia.

Baada ya sakata hilo Kupitia ukurasa Wake wa Instagram, Diamond Platnumz aliposti video hiyo na kuandika:

https://www.instagram.com/p/BrK67ZVlDFX/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=d9geezbdwlgj

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.