Diamond: Sijawahi Kulipa Kufanya Kolabo Na Msanii Yoyote Wa Marekani Wenyewe Wananikubali

Mwanamuziki wa Bongo fleva, Diamond Platnumz anayezidi kufanya vizuri na ngoma yake ya ‘hallelujah’ amezidi kutengeneza headlines baada ya kushirikisha wasanii wakubwa kwenye nyimbo zake.

Diamond ambaye ni juzi tu ametoka kufanya video ya wimbo wake atakao mshirikisha mwanamuziki kutoka Marekani Omarion, pia wiki chache zilizopita ametoka nchini Marekani kwaajili ya kolabo yake na msanii na rapa maarufu kutoka Marekani Rick Ross. Pia mbali na hao wote ni juzi tu Diamond katoka kupokea tuzo yake baada ya mauzo ya nyimbo yake aliomshirikisha mwanamuziki mwingine kutoka Marekani ambaye ni Neyo, kufikisha platnum mara sita.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyoyafanya na dizzim tv Diamond alifunguka na kudai kuwa hajawahi kuwalipa hats senti wasanii hao wote wala hawafati bali wao wanaona kazi zake na wanavutiwa na kumtafuta:

Mimi sijawahi kulipia kufanya kolabo na msanii yoyoye wa Marekani, na ukichunguza kiundani kolabo zangu na Wamarekani sio kitu ambacho nimejishobokesha ni watu ambao wanatakiwa kunikubali na kuupenda mziki ninaofanya ili waweze kufanya kazi na mimi ndio maana sometimes unaona kuwa siposti nikiwa nao kwasababu wao wenyewe wanafurahi na wanapenda kuposti na pia naogopa kuposti nisije kuonekana najishaua wakati hiyo sio pointi yangu mimi nachotaka ni kuuchukua mziki wa Bongo fleva kuupeleka mbele”.

Pia Diamond aliongelea album yake mpya inayokuja hivi karibuni inayoitwa ‘A boy from Tandale’ aliowashirikisha wasanii mbali mbali ndani ya Afrika na nje ya Afrika na itahusu mambo mengi kama maisha yake binafsi na nchi ya Tanzania kwa ujumla.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.