Dogo Janja Akimbilia Kwa Mwanasaikolojia.
Msanii wa muziki wa bongo fleva Dogo Janja ameanza kuonekana akitafuta msaada kwa kile kilichodaiwa kuwa anahitaji msaada wa kisaikolojia kutoka na matatizo ya msongo wa mawazo unaomkumba hasa baada ya kushindwa kukubaliana na hali halisa ya mahusianoa yake.
Mwanamuziki huyo ambae aliweka picha yake akiwa na mwanasaikolojia Chris Mauki, imesemekana kuwa hali yake kwa sasa haiko sawa hivyo imembidi kutafuta msaada zaidi.
Kama utakumbuka basi wiki chache zilizopita, mwanamuziki huyo aliwahi kuripotiwa kuwa mgonjwa hospitali huku sababu kubwa ikisemekana kuwa ni msongo wa mawazo wa kusindwa kukubaliana na hali halisi ya mfarakano wake na mkewe.
Hata hivyo Uwoya mwenyewe amekuwa akikanusha taarifa hizo ilhali kumekuwa hakua zile rapsha rapsha za mapenzi kama ilivyokuwa hapo awali kati yao.